Sisi Kama Sisi

Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatuna elimu lakini ni wajuaji 
Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatutaki kutembea bali kukimbia
 Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatushibi, 
Tunakula mpaka tunajamba 
Tuna ujeuri usiokuwa na faida
Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida 
Na tunaona ni sawa tu.

Tatizo letu sisi kama sisi ni wanafiki, Tunasema ndio kumbe tunamaanisha la
Tatizo letu sisi kama sisi ni wavivu, hatuoni maana ya kuchapa kazi, Sio kufanya kazi bali kuchapa kazi Tuna ujeuri usiokuwa na faida
Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida
Na tunaona ni sawa tu.

Tatizo letu sisi kama sisi hatupendani, Tunathamini watu wa nje kuliko wa ndani Chakushangaza hata hawa ndugu zetu kina nyani Huwa wanapeana heshima fulani
Tuna ujeuri usiokuwa na faida
Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida
Na tunaona ni sawa tu.

Sisi kama sisi hatuwezi kuendelea
Maana tayari kizazi chetu kimeshapotea
Wale waliobaki kazi yao kubwa ni kuwaonea na kuwatendea wale wenzao wanao wategemea 
Ule ujeuri usiokuwa wa kawaida na faida sasa umebaki kutuzomea
Na tunaona ni sawa tu.

© SMS
Copyright © | Year Posted 2015

Poem

Post Comments

Poetrysoup is an environment of encouragement and growth so only provide specific positive comments that indicate what you appreciate about the poem. Negative comments will result your account being banned.

Please Login to post a comment

Be the first to comment on this poem. Encourage this poet.

Get a Premium Membership
Turn off ads, get more exposure for your poetry, and get more features with a Premium Membership.
Book: Diverse Voices: The Poetry of Human Rights and the Pursuit of Peace