Get Your Premium Membership

Sisi Kama Sisi

Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatuna elimu lakini ni wajuaji Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatutaki kutembea bali kukimbia Tatizo letu sisi kama sisi ni kwamba hatushibi, Tunakula mpaka tunajamba Tuna ujeuri usiokuwa na faida Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida Na tunaona ni sawa tu. Tatizo letu sisi kama sisi ni wanafiki, Tunasema ndio kumbe tunamaanisha la Tatizo letu sisi kama sisi ni wavivu, hatuoni maana ya kuchapa kazi, Sio kufanya kazi bali kuchapa kazi Tuna ujeuri usiokuwa na faida Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida Na tunaona ni sawa tu. Tatizo letu sisi kama sisi hatupendani, Tunathamini watu wa nje kuliko wa ndani Chakushangaza hata hawa ndugu zetu kina nyani Huwa wanapeana heshima fulani Tuna ujeuri usiokuwa na faida Tuna ujeuri usiokuwa wa kawaida Na tunaona ni sawa tu. Sisi kama sisi hatuwezi kuendelea Maana tayari kizazi chetu kimeshapotea Wale waliobaki kazi yao kubwa ni kuwaonea na kuwatendea wale wenzao wanao wategemea Ule ujeuri usiokuwa wa kawaida na faida sasa umebaki kutuzomea Na tunaona ni sawa tu. © SMS

Copyright © | Year Posted 2015




Post Comments

Poetrysoup is an environment of encouragement and growth so only provide specific positive comments that indicate what you appreciate about the poem. Negative comments will result your account being banned.

Please Login to post a comment

A comment has not been posted for this poem. Encourage a poet by being the first to comment.


Book: Reflection on the Important Things