Shoga Atoka Ulaya
Juzi juzi tulikuwa tunakutana
Kwenye mishwari tulipitana
Hili na lile tuliambiana
Menzangu ukaenda majuu
Kufika kule ukajiona wewe mungu
Uliotuacha huku nyuma ukatufananisha na vyungu
Haya yote yalinifanya nihisi uchungu
Lakini usijali siku hadi siku Nitarudisha zangu nguvu.
Umerudi jana, kimya kimya unaogopa kurogwa
Waache kurogwa wenye mahela Urogwe wewe hombolela
Kwa maalim ulifika
Dua na ubani ukaoshwa
Macho ya watu yasije kukudhuru Maana wewe ni kama nuru Kilaupitapo mwanga unazidi kuwaka
Shoga hatukuwezi
Huko majuu itabidi tufike
Hata kama kukifika kama wezi.
Leo tumegongana
Excuse me ukanitamkia
Kiswahili umesahau
Barabara zina vumbi sana
Watu huwawezi
Uswazi umewazidi
Sana wamekuwa wakaaidi
Maneno wanayo ongea unaona kwako si sahihi Sana sana unawalinganisha na watu wa chini
?Kila ukimaliza kuamkia
Mkono wako unaosha na sabuni
Maradhi ya uswazi unayaogopa
Usije ukarudi ‘kwenu’ na magonjwa ya kuporomoka
Kwa majembe na mashoka
Unagamba kama mungu kakupa vyema ya kuokoka
Shoga umetisha
Huko majuu mwenzagu hatusemi
Leo kunisalimia unaona tabu
Mila za kwetu kwako unaona kavu
Kila usimamapo unahesabu hadi tatu
Asije mshenzi kukupora ukahisi moyo umekuwa mchafu Maana huku kwetu wezi kweli ni tabu
Shoga tangu umerudi kutoka ulaya, hatukuwezi
Nakupa miaka kama kumi
Umalize katabia kauhuni
Umalize ulaya kuwachuna
Uje huku tukucheke
Maendeleo uliokuwa unayataka yamekupiga teke Aibu unawakataza kwenu wasipayuke Kwakeli wewe mtoto wa kike
Kubali yakubalike
Nafsi yako ifanye impumzike
Copyright © Shamsa Suleiman | Year Posted 2015
Post Comments
Poetrysoup is an environment of encouragement and growth so only provide specific positive comments that indicate what you appreciate about the poem.
Please
Login
to post a comment