Get Your Premium Membership

Shoga Atoka Ulaya

Juzi juzi tulikuwa tunakutana 
Kwenye mishwari tulipitana
Hili na lile tuliambiana
Menzangu ukaenda majuu
Kufika kule ukajiona wewe mungu 
Uliotuacha huku nyuma ukatufananisha na vyungu 
Haya yote yalinifanya nihisi uchungu
Lakini usijali siku hadi siku Nitarudisha zangu nguvu.

Umerudi jana, kimya kimya unaogopa kurogwa 
Waache kurogwa wenye mahela Urogwe wewe hombolela
Kwa maalim ulifika
Dua na ubani ukaoshwa
Macho ya watu yasije kukudhuru Maana wewe ni kama nuru Kilaupitapo mwanga unazidi kuwaka
 Shoga hatukuwezi
Huko majuu itabidi tufike
Hata kama kukifika kama wezi.

Leo tumegongana
Excuse me ukanitamkia
Kiswahili umesahau
Barabara zina vumbi sana
Watu huwawezi
Uswazi umewazidi
Sana wamekuwa wakaaidi
Maneno wanayo ongea unaona kwako si sahihi Sana sana unawalinganisha na watu wa chini

?Kila ukimaliza kuamkia
Mkono wako unaosha na sabuni
Maradhi ya uswazi unayaogopa
Usije ukarudi ‘kwenu’ na magonjwa ya kuporomoka
 Kwa majembe na mashoka
Unagamba kama mungu kakupa vyema ya kuokoka
 Shoga umetisha
Huko majuu mwenzagu hatusemi

Leo kunisalimia unaona tabu
Mila za kwetu kwako unaona kavu
Kila usimamapo unahesabu hadi tatu
Asije mshenzi kukupora ukahisi moyo umekuwa mchafu Maana huku kwetu wezi kweli ni tabu
Shoga tangu umerudi kutoka ulaya, hatukuwezi

Nakupa miaka kama kumi
Umalize katabia kauhuni
Umalize ulaya kuwachuna
Uje huku tukucheke
Maendeleo uliokuwa unayataka yamekupiga teke Aibu unawakataza kwenu wasipayuke Kwakeli wewe mtoto wa kike
Kubali yakubalike
Nafsi yako ifanye impumzike

Copyright © | Year Posted 2015




Post Comments

Poetrysoup is an environment of encouragement and growth so only provide specific positive comments that indicate what you appreciate about the poem. Negative comments will result your account being banned.

Please Login to post a comment

Date: 1/22/2016 9:16:00 PM
SHAMSA, Enjoyed the way you expressed every line. Always with LUV **SKAT
Login to Reply
Date: 12/7/2015 4:23:00 AM
ahsante, do the words have meaning
Login to Reply
Date: 12/6/2015 11:50:00 PM
sounds nice. is it spontaneous expression or a language
Login to Reply
Suleiman Avatar
Shamsa Suleiman
Date: 12/7/2015 4:14:00 AM
Ahsante Francis, It is an expression. Sort of a mirror of how individuals respond to loved ones when they change. A bit of anger, anxiety, jealousy and longing.

Book: Reflection on the Important Things