Spasiba- Ian Munywe
SPASIBA
Spasiba,
spasiba.
Kwa mwenyezi,
bila kipimo nakuenzi.
Spasiba,
spasiba.
Kwa mama ulileta duniani,
na kunilea.
Spasiba,
spasiba.
Kwa marafiki wa kikweli,
sio wahuni.
Spasiba,
spasiba.
Kwa wahusika wote wenye nia njema,
sio wenye sumu kwenye sindano.
Spasiba,
spasiba.
Kwa maadui washirikina na wenye fitina,
wasio na utu ila tu unafiki.
Garagazano hili,
hamwezi.
Spasiba,
spasiba.
LiterarySpaceAfrica Ian Munywe©
Copyright © Ian Munywe | Year Posted 2018
Post Comments
Poetrysoup is an environment of encouragement and growth so only provide specific positive comments that indicate what you appreciate about the poem.
Please
Login
to post a comment